11Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
13Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
14Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.