4Ndipo utapata kibali na heshima mbele Mungu na wanadamu.
5Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote na wala usitegemee ufahamu wako mwenyewe,
6katika njia zako zote mkiri Yeye na yeye atayanyosha mapito yako.
7Usiwe mwenye busara machoni pako mwenyewe; mche Yehova na jiepushe na uovu.
8Itakuponya mwili wako na kukuburudisha mwili wako.
9Mheshimu Yehova kwa utajiri wako na kwa malimbuko ya mazao kwa kila unachozalisha,
10na ndipo ghala zako zitajaa na mapipa makubwa yatafurika kwa divai mpya.
11Mwanangu, usidharau kuadibishwa na Yohova na wala usichukie karipio lake,
12maana Yehova huwaadibisha wale wapendao, kama baba anavyoshughulika kwa mtoto wake ampendezaye.
13Yeye apataye hekima anafuraha, naye hupata ufahamu.
14Kwani katika hekima unapata manufaa kuliko ukibadilisha kwa fedha na faida yake inafaa zaidi kuliko dhahabu.