3Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
4Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
5Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
6Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
7Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
8Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.