Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 31

Mithali 31:17-27

Help us?
Click on verse(s) to share them!
17Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
18Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
19Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
20Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
21Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
22Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
23Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
24Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
25Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
26Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
27Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.

Read Mithali 31Mithali 31
Compare Mithali 31:17-27Mithali 31:17-27