10Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
12Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
13Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
14Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.