6Usiyaongezee maneno haya, au atakukemea, na utathibitishwa kuwa mwongo.
7Vitu viwili ninakuomba, usivikatalie kwangu kabla sijafa:
8Majivuno na uongo viweke mbali nami. Usinipe umasikini wala utajiri, nipe tu chakula ninachohitaji.
9Maana nikipata vingi zaidi, nitakukana wewe na kusema, “Yehova ni nani?” Au kama nitakuwa masikini, nitaiba na kukufuru jina la Mungu wangu.