21Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
24Vitu vinne duniani ni vidogo na bado vinabusara: