Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 2

Mithali 2:8-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8huongoza katika njia za haki na atalinda njia ya waaminifu kwake.
9Ndipo utakapoelewa wema, haki, usawa na kila njia njema.
10Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
12Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
13Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
14Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
15Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.

Read Mithali 2Mithali 2
Compare Mithali 2:8-15Mithali 2:8-15