Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 26

Mithali 26:1-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.

Read Mithali 26Mithali 26
Compare Mithali 26:1-10Mithali 26:1-10