Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 25

Mithali 25:20-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
20Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.

Read Mithali 25Mithali 25
Compare Mithali 25:20-25Mithali 25:20-25