7Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.