5Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.