5Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.