23Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.