Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 24

Mithali 24:18-32

Help us?
Click on verse(s) to share them!
18au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.

Read Mithali 24Mithali 24
Compare Mithali 24:18-32Mithali 24:18-32