Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 24

Mithali 24:11-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
11Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
13Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.

Read Mithali 24Mithali 24
Compare Mithali 24:11-16Mithali 24:11-16