21maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.