17Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.