7Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.