Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:9-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:9-15Mithali 21:9-15