14Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.