12Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.