5Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
6Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
7Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
8Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
9Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.