Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 18

Mithali 18:15-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
16Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
17Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
18Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
19Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
20Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
21Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.

Read Mithali 18Mithali 18
Compare Mithali 18:15-21Mithali 18:15-21