7Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
10Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
11Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.