26Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.