6Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
7Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
8Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.