Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 15

Mithali 15:18-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
18Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
19Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
20Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
21Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
22Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
23Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
24Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu.
25Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.

Read Mithali 15Mithali 15
Compare Mithali 15:18-25Mithali 15:18-25