2Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.