Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 11

Mithali 11:8-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Yule atendaye haki hulindwa katika taabu na badala yake taabu humjia mwovu.
9Kwa kinywa chake asiyeamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa wale watendao haki hulindwa salama.
10Wanapofanikiwa watendao haki, mji hufurahi, waovu wanapoangamia, kunakuwa na kelele za furaha.
11Kwa zawadi nzuri za wale wanaompendeza Mungu, mji unakuwa mkubwa; kwa kinywa cha waovu mji huvurugwa.
12Mtu mwenye dharau kwa rafiki yake hana akili, bali mtu mwenye ufahamu hunyamaza.
13Anayekwenda akizunguka kwa kukashifu hufunua siri, bali mtu mwaminifu hustiri jambo.
14Pasipokuwa na uongozi wenye busara, taifa huanguka, bali ushindi huja kwa kushauriana washauri wengi.
15Anayemdhamini mkopo wa mgeni ataumia kwa usumbufu, bali anayechukia kutoa rehani kwa namna ya ahadi yupo salama.
16Mwanamke mwenye rehema hupata heshima, bali watu wakorofi hufumbata utajiri.

Read Mithali 11Mithali 11
Compare Mithali 11:8-16Mithali 11:8-16