Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 23

Luka 23:13-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
17Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
19(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”

Read Luka 23Luka 23
Compare Luka 23:13-22Luka 23:13-22