Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 23

Luka 23:13-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
14Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
15Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
16Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
17(Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
18Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
19Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
20Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
21Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
22Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”

Read Luka 23Luka 23
Compare Luka 23:13-22Luka 23:13-22