Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Luka 23:13-22 in Swahili (individual language)

Help us?

Luka 23:13-22 in Biblia Takatifu

13 Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14 akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15 Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16 Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
17 Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
19 (Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20 Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21 lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22 Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
Luka 23 in Biblia Takatifu

Luka 23:13-22 in Biblia ya Kiswahili

13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
Luka 23 in Biblia ya Kiswahili