Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 4

Luka 4:14-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
14Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”

Read Luka 4Luka 4
Compare Luka 4:14-21Luka 4:14-21