Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 11

Hesabu 11:2-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Ndipo watu wakamwita Musa kwa nguvu, Naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukazimika.
3Mahali pale paliitwa Tabera, kwa sababu moto wa BWANA uliwaka kati yao.
4Baadhi ya wageni wakaanza kuweka kambi zao pamoja na wana wa wa Israeli. Walitaka kula chakula kizuri. Kisha wana wa Israeli walipoanza kulia wakisema, “Ni nani atakayetupatia nyama za kula?
5Tunakumbuka samaki tulizokula bure kule Misri, yale matango, na matikiti maji, na mboga na vitunguu na vitunguu saumu.
6Na sasa hatuna hamu ya kula, kwa sababu tunaona mana tu.
7Mana ilifanana na punje ya mtama. ilionekana kama bedola.
8watu wakazunguka kisha wakakusanyika. Wakaisaga, wakaitwanga kwa vinu, wakaitokosa nyunguni, na kuitengeneza mikate. radha yake ilikuwa kama mafuta mapya ya mizeituni.
9Na umande ulipoanguka kambini usiku ule, na mana ilianguka pia.

Read Hesabu 11Hesabu 11
Compare Hesabu 11:2-9Hesabu 11:2-9