Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 10

Hesabu 10:10-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Pia, wakati wa kusherehekea, sikukuu zenu za kawaida na katika miandamo ya miezi, mtapiga tarumbeta zenu kwa heshima ya sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani. Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu, Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
11Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
12Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
13Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
14Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
15Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
16Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.

Read Hesabu 10Hesabu 10
Compare Hesabu 10:10-16Hesabu 10:10-16