15Siwaombei kwamba uwatoe ulimwenguni bali uwalinde na yule mwovu.
16Wao si wa dunia kama vile mimi nisivyokuwa wa ulimwenguni.
17Uwaweke wakfu kwako mwenyewe katika Kweli; neno lako ndiyo kweli.
18Ulinituma ulimwenguni, nami nimewatuma ulimwenguni.
19Kwa ajili yao mimi mwenyewe ninajitoa kwako ili kwamba na wao wajitoe kwako kwa ile kweli.
20Si hawa tu ninaowaombea, bali na wale watakaoamini kupitia neno lao
21ili kwamba wao nao wawe na umoja, kama vila wewe Baba, ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Nawaombea ili kwamba wao pia waweze kuwa ndani yetu ili ulimwengu uweze kuamini kuwa wewe ndiye uliyenituma.