Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 17

Yohana 17:15-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Siombi uwatoe ulimwenguni, bali naomba uwakinge na yule Mwovu.
16Wao si wa ulimwengu, kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
17Waweke wakfu kwa ukweli; neno lako ni ukweli.
18Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, nami pia nimewatuma wao ulimwenguni;
19na kwa ajili yao mimi mwenyewe najiweka wakfu ili nao pia wafanywe wakfu katika ukweli.
20“Siwaombei hao tu, bali nawaombea pia wote watakaoamini kutokana na ujumbe wao.
21Naomba ili wote wawe kitu kimoja. Baba! Naomba wawe ndani yetu kama vile wewe ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Naomba wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ulinituma.

Read Yohana 17Yohana 17
Compare Yohana 17:15-21Yohana 17:15-21