Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 1

Luka 1:54-65

Help us?
Click on verse(s) to share them!
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.”
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:54-65Luka 1:54-65