25Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
26Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
27Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
28Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.