Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 10

Hesabu 10:29-34

Help us?
Click on verse(s) to share them!
29Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
30Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
31Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
32Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
33Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
34Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.

Read Hesabu 10Hesabu 10
Compare Hesabu 10:29-34Hesabu 10:29-34