Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Hesabu 10:29-34 in Swahili (individual language)

Help us?

Hesabu 10:29-34 in Biblia ya Kiswahili

29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
34 Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.
Hesabu 10 in Biblia ya Kiswahili