Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 10

Hesabu 10:15-34

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
16Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
17Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
18Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
19Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
20Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
21Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
22Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
23Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
24Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
25Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
26Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
27Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
28Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
29Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
30Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
31Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
32Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
33Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
34Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.

Read Hesabu 10Hesabu 10
Compare Hesabu 10:15-34Hesabu 10:15-34