13Yapata watu watu elfu arobaini walioandaliwa kwa vita walipita mbele za Yahweh, kwa ajili ya vita katika uwanda wa Yeriko.
14Katika siku hiyo Yahweh alimfanya Yoshua kuwa mkuu katika macho ya watu wote wa Israeli. Walimheshimu - kama walivyomheshimu Musa - siku zake zote.
15Kisha Yahweh akamwambia Yoshua,
16“Waamuru makuhani wanaolibeba sanduku la ushuhuda watoke katika Yordani.”
17Hivyo Yoshua akawaamuru makuhani, “pandeni mtoke Yordani.”