Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Marko - Marko 8

Marko 8:22-26

Help us?
Click on verse(s) to share them!
22Yesu alifika Bethsaida pamoja na wanafunzi wake. Huko watu wakamletea kipofu mmoja, wakamwomba amguse.
23Yesu akamshika mkono huyo kipofu, akampeleka nje ya kijiji. Akamtemea mate machoni, akamwekea mikono, akamwuliza, “Je, unaweza kuona kitu?”
24Huyo kipofu akatazama, akasema, “Ninawaona watu wanaoonekana kama miti inayotembea.”
25Kisha Yesu akamwekea tena mikono machoni, naye akakaza macho, uwezo wake wa kuona ukamrudia, akaona kila kitu sawasawa.
26Yesu akamwambia aende zake nyumbani na kumwamuru, “Usirudi kijijini!”

Read Marko 8Marko 8
Compare Marko 8:22-26Marko 8:22-26