8Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
9Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata.”
10Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
11Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
12Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umeponywa ugonjwa wako.”