Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Luka 13:8-12 in Swahili (individual language)

Help us?

Luka 13:8-12 in Biblia Takatifu

8 Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
9 Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata.”
10 Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
11 Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
12 Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umeponywa ugonjwa wako.”
Luka 13 in Biblia Takatifu

Luka 13:8-12 in Biblia ya Kiswahili

8 Mtunza bustani akajibu na kusema, 'uache mwaka huu ili niupalilie na kuweka mbolea juu yake.
9 Kama ukizaa matunda mwaka ujao, ni vema; lakini kama hautazaa, uukate.!”'
10 Sasa Yesu alikuwa akifundisha katika mojawapo ya Masinagogi wakati wa Sabato.
11 Tazama, alikuwepo mama mmoja ambaye kwa miaka kumi na minane alikuwa na rohomchafu wa udhaifu, na yeye alikuwa amepinda na hana uwezo kabisa wa kusimama.
12 Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umewekwa huru kutoka kwenye udhaifu wako.”
Luka 13 in Biblia ya Kiswahili