Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Marko - Marko 8

Marko 8:24-32

Help us?
Click on verse(s) to share them!
24Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
25Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
26Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
27Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
28Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
29Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
30Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
31Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
32Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.

Read Marko 8Marko 8
Compare Marko 8:24-32Marko 8:24-32