Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 6

Luka 6:22-29

Help us?
Click on verse(s) to share them!
22Mmebarikiwa ninyi ambao watu watakapowachukia na kuwatenga na kuwashutumu ninyi kwamba ni waovu, kwa ajili ya Mwana Adamu.
23Furahini katika siku hiyo na kurukaruka kwa furaha, kwa sababu hakika mtakuwa na thawabu kubwa mbinguni, kwa maana baba zao waliwatendea vivyohivyo manabii.
24Lakini ole wenu mlio matajiri! Kwa maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Ole wenu mlio shiba sasa! Kwa maana mtaona njaa baadaye. Ole wenu mnaocheka sasa! Kwa maana mtaomboleza na kulia baadaye.
26Ole wenu, mtakaposifiwa na watu wote! Kwa maana baba zao waliwatendea manabii wa uongo vivyohivyo.
27Lakini nasema kwenu ninyi mnaonisikiliza, wapendeni adui zenu na kufanya mema kwa wanao wachukieni.
28Wabarikini wale wanao walaani ninyi na waombeeni wale wanaowaonea.
29Kwake yeye akupigaye shavu moja, mgeuzie na la pili. Kama mtu akikunyang'anya joho lako usimzuilie na kanzu.

Read Luka 6Luka 6
Compare Luka 6:22-29Luka 6:22-29