Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 22

Luka 22:43-49

Help us?
Click on verse(s) to share them!
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”

Read Luka 22Luka 22
Compare Luka 22:43-49Luka 22:43-49